UDOM WASHIRIKI MAONESHO YA VYUO VIKUU KATIKA VIWANJA VYA KARIMJEE - PATRICIA-TV.com

Breaking

Share daily activities and have all funs here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Saturday, July 23, 2016

UDOM WASHIRIKI MAONESHO YA VYUO VIKUU KATIKA VIWANJA VYA KARIMJEE


Mhadhiri Msaidizi kutoka chuo kikuu cha Dodoma, Lucian Ngeze akitoa ufafanuzi kuhusu kutenga matumizi ya LUKU ya nyumba moja kadili ya matumizi ya kila mtu.


Mhadhiri kutoka college ya Education chuo kikuu cha Dodoma, Dk. Pambasi Tandika akimsikiliza mwanafunzi baada ya kumweleza jinsi ya kujiunga chuoni hapo wakati wa maonesho ya vyuo vikuu yaliyoshirikisha vyuo mbalimbali hapa nchini.

CHUO kikuu cha Dodoma chashiriki Maonesho ya Vyuo vikuu hapa nchini yanayoendelea kufanyika katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam, ambayo yatafanyika kwa takribani siku tatu kuanzia leo Julai 20 hadi Julai 22 mwaka huu.

Katika maenesho hayo Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako ametembelea mabanda mbalimbali katika maonesho hayo ya Vyuo Vikuu (TCU)


Mhadhiri Msaidizi kutoka college ya CIVE chuo kikuu cha Dodoma, Ms Tulibako Tulibonywa akitoa ufafanuzi mbele ya vijana waliotembelea kwenye banda la chuo hicho leo


Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma, Kadaso Kipingili (Mwenye Tshirt Nyeupe) akitoa ufafanuzi kuhusu maelezo kwa wananchi waliofika katika banda la chuo kikuu cha Dodoma leo wakati wa maonesho ya Vyuo vikuu yaliyoandaliwa na TCU.


Baadi ya wanafunzi wakisoma majarida kutoka chuo kikuu cha Dodoma leo katika maonesho.


Afisa Tawala, Idara ya Utafiti na Machapisho kutoka chuo kikuu cha Dodoma akiwaonesha vijana jinsi ya kujiunga pamoja na kuwaeleza vigezo vya kujiunga na Chuo hicho.


Mhadhiri wa chuo kikuu cha Dodoma, Teng Peng akiwaonesha baadi ya vijana waliofika kwenye banda la Udom Comfusious



Baadhi ya mitambo iliyotengenezwa na wanachuo wa chuo kikuu cha Dodoma ambayo inaweza kuongoza magari kwa kutumia umeme wa nguvu ya Jua.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here