Mkali wa Hip Hop Kalla Jeremiaha ameongea na Enews na kueleza sababu zinazopelekea yeye kuonekana kama amepotea kwenye muziki na kusema sio kweli kwamba kapotea bali ni kwa sababu za kujiweka mbali na kiki zisizo na msingi.
Hata hivyo Kalla ameelezea jina la mtoto wake ambaye ni takribani miezi 3 tangu azaliwe huku akitoa sababu zilizopelekea yeye kumuita mtoto wake “ALAMA” na kusema ni neno la kiswahili na kwamba anadumisha lugha yake kwani angemuita kwa lugha ya kingereza jina lake lingekuwa 'Mark'
Amesema jina hilo halijaleta matatizo yoyote kwa mtoto wake tofauti na watu wanavyosema usipomuita mtoto jina la asili anakuwa anasumbua kwa kulia au kuumwaumwa ila kwa mtoto wa Kalla imekuwa tofauti kabisaa.
No comments:
Post a Comment