LIONEL MESSI AHUKUMIWA KUFUNGWA JELA - PATRICIA-TV.com

Breaking

Share daily activities and have all funs here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Wednesday, July 6, 2016

LIONEL MESSI AHUKUMIWA KUFUNGWA JELA


Mchezaji nyota wa Argentina na Barcelona Lionel Messi amehukumiwa kifungo cha miezi 21 jela baada ya kupatikana na makosa ya kutumia ulaghai wakati wa ulipaji ushuru, vyombo vya habari nchini Uhispania vinaripoti.

Babake, Jorge Messi, pia amehukumiwa kufungwa jela kwa kuilaghai Uhispania €4.1m (£3.2m; $4.6m) kati ya 2007 na 2009.

Wakati wa kesi, waendesha mashtaka walisema maeneo salama yenye kinga dhidi ya ushuru Belize na Uruguay yaliyumiwa kuficha mapato kutokana na uuzaji wa haki za picha za mchezaji huyo.

Lakini Messi amesema hakufahamu lolote kuhusu masuala yake ya kifedha. Wawili hao hata hivyo hawatarajiwi kufungwa jela.

Chini ya mfumo wa haki nchini Uhispania, mtu anaweza kutumikia kifungo chochote kilicho chini ya miaka miwili nje ya gereza.

Messi na babake pia wanaweza kukata rufaa katika Mahakama ya Juu nchini humo.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here